Mwigulu Nchemba ameifananisha Singida United na Club ya England - boazmwakasege.com

MADA MOTO

Sunday, February 12, 2017

Mwigulu Nchemba ameifananisha Singida United na Club ya England

Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba ambaye aliwaongoza mashabiki lukuki wa Singida kuishangilia timu yao ya Singida United ambapo imefanikiwa kupanda ligi kuu msimu ujao baada ya kuifunga Alliance 2-0 amesema, Singida United itakuwa kama Leicester City ya England ambayo ilipanda ligi kuu na kutwaa taji la ligi kwa kuvibwaga vigogo.

“Ninafuraha sana kama ambavyo unawaona wanasingida, hili ni jambo ambalo limesubiriwa kwa miaka mingi sana na sisi kama wadu wa mkoa wa Singida tutaendelea kuunga mkono timu yetu ya mkono timu yetu ya mkoa ili iweze kufanya vizuri zaidi,” – Mwigulu Nchemba.

“Nawatakiwa kila la heri wana Singida, tuendelee kuiunga mkono timu yetu ya Singida United. Msimu ujao Singida United itakuwa kama Leicester City, inaenda kuchukua ubingwa.”


Nchemba ni mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi na mdau mkubwa wa soka nchini akiziunga mkono Singida United ya mkoani Singida pamoja na Yanga SC.

No comments:

Post a Comment