Gurdiola kupunguza 12 na kutumia £200M kuleta wapya. - boazmwakasege.com

MADA MOTO

Friday, February 10, 2017

Gurdiola kupunguza 12 na kutumia £200M kuleta wapya.


Pep Gurdiola anaendelea kuonekana wakawaida akiwa Uingereza.Tofauti na alipokuwa Hispania na baadae Ujerumani Pep haonekani kuwa na makali yaleyale ya alikotoka.Man City wamekuwa hawaeleweki msimu huu na kidogo ujio wa bwanamdogo Gabriel Jesus amewaokoa wikiendi iliyopita.

Sasa baada ya Gurdiola kuona hali inazidi kuwa mbaya Man City ameamua kufanya maamuzi magumu.Taarifa zinasema Pep anataka kupunguza wachezaji 12 katika kikosi chake na kuleta wapya.Pep Gurdiola anaona wachezaji wengi wa City hawaendani na mfumo wake hivyo inabidi aondoke.

Inajulikana kwamba mshambuliaji wa Man City Kun Aguero ameanza kupoteza namba kwa Jesus.Katika mechi mbili mfululizo zilizopita Aguero alikaa jukwaani akimuangalia Jesus akifunga tu.Sio rahisi kwa mshambuliaji aliye na kiwango cha Aguero kukubali kusota jukwaani,anaweza kuwa mmoja ya wachezaji wanaoondoka.

Lakini Bravo pia golikipa wao pamoja na Yaya Toure japo anacheza lakini hana uhusiano mzuri sana na Pep na hii inaweza kumfanya aondoke.Gurdiola amekuwa akiamini sana vijana wadogo hasa katika timu ya City kwani unaweza kuona Sane,Sterling na Jesus walivyoweza kuaminika na kweli kuanza kuleta matokeo.Hii inamaanisha wachezaji wenye umri mkubwa wanaweza kufunguliwa mlango wa kutokea katika dirisha lijalo la usajili.


Wakati Gurdiola akipunguza watu lakini tayari ametenga £ 200m kwa ajili ya usajili.Na inafahamika Gurdiola anataka kusajili mabeki wawili,kiungo mmoja na striker.Mabeki wamekuwa tatizo kwake kwani beki wao Stones waliyemsajili kutoka Everton siku za usoni amekuwa akiigharimu sana timu kwa makosa yake na pia muunganiko wake na Otamendi umekuwa hauelewani.Lazima Gurdiola atatafuta mtu wa kuja kukaa na Stones kama pacha au kujenga upya kabisa eneo la beki.
Ikey Gundogan nae alikuja City akiwa na majeruhi ambayo bado yanamuandama na kushindwa kucheza.Inaonekna Gurdiola anampenda Gundogan tofauti na viungo wengine aliowakuta City.Lakini ameshindwa kabisa kumtumia na sasa ni dhahiri Gurdiola atatafuta kiungo mwingine ambae anafanana kiuchezaji na Ikey Gundogan.


Katika upande wa ushambuliaji imeripotiwa mara kadhaa City walijaribu kumuunganisha Gurdiola na mchezaji wake wa zamani Lioneil Messi.City bado wanahusishwa na usajili huo ambao unaweza kuvunja rekodi ya dunia na hata kama sio Messi bado Gurdiola anahitaji mtu wa kuwapa changamoto washambuliaji wake wa sasa.

No comments:

Post a Comment