Rekodi ya John Bocco dhidi ya Simba utaipenda…. - boazmwakasege.com

MADA MOTO

Saturday, January 28, 2017

Rekodi ya John Bocco dhidi ya Simba utaipenda….

Image result for john bocco vs simba sc

Bocco ndiye mshambuliaji pekee nchini mpaka sasa aliyeweza kuzitesa timu za Simba na Yanga kwa kufunga mabao, kila anapokutana nazo katika mechi mbalimbali.

Ukiondoa rekodi ya kuifunga Yanga jumla ya mabao 12, Bocco mpaka sasa amefanikiwa kutikisa nyavu za Simba mara 18 katika mechi za mashindano mbalimbali ambapo John Bocco kutoka Azam FC leo ameisaidia timu yake ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba Sport Club katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam. Na kumfanya awe ametikisa nyavu za Simba mara 19.


Bocco aliingia kwenye mchezo huo dhidi ya Simba  akiwa na morali kubwa ya kuendeleza rekodi yake ya kufunga kwani katika mechi ya mzunguko wa kwanza msimu uliopita alitupia mawili kwenye sare ya 2-2, huku ya wekundu hao yakifungwa na Ibrahim Ajib.

No comments:

Post a Comment