Viini tete ambavyo ni 0.001% binadamu na sehemu iliyosalia
ni nguruwe, vimekuzwa na wanasayansi nchini Marekani.
Hicho ni kisa cha kwanza kwa viumbe ambao ni mseto wa
binadamu na viumbe wengine kuzalishwa kwa kuunganisha sehemu kutoka kwa
binadamu na viumbe vingine.
Lengo limekuwa kujaribu kubaini iwapo inawezekana viungo vya
binadamu kukuzwa kwenye wanyama.
Watoto kuzaliwa na wazazi watatu Uingereza
Nyota wa filamu India abeba nguruwe kwenye benki
Hata hivyo, makala ya kisayansi iliyoandikwa kwenye jarida
la Cell inaonyesha shughuli hiyo ina changamoto nyingi.
Makala hiyo imeelezwa kuwa "ya kusisimua sana" na
watafiti wengine.
Ilii kuunda kiini tete kama hicho ambacho kimepewa jina
kimaira (Chimera), - ambaye ni mnyama katika hadithi mwenye kichwa cha simba,
mwili wa mbuzi na mkia wa nyoka, atokaye moto kinywani - wataalamu walitumia
seli tete (seli zinazoweza kukua kuwa seli za aina yoyote mwilini) na kuziweka
ndani ya kiini tete cha nguruwe.
Kiini tete hicho - ambacho sasa kimechanganyikana seli za
binadamu na nguruwe - kiliwekwa ndani ya nyumba ya uzazi ya nguruwe jike na kukaa
kwa mwezi mmoja.
Shughuli hiyo hata hivyo ilikuwa na changamoto nyingi na
kati ya viini tete 2,075 vilivyowekwa ndani ya nguruwe, ni viinitete 186
vilivyokuwa hadi siku ya 28.
Hata hivyo, kulikuwa na dalili za matumaini kwamba seli za
binadamu zilikuwa bado zinakuwa, ingawa ziliunda sehemu ndogo sana ya viungo
vya mwili kwenye kiinitete hicho kilichochanganyikana seli za nguruwe na
binadamu.
No comments:
Post a Comment