AY kwa maneno yake mwenyewe, si mtu anayependa kufanya kitu kile kile muda wote akitarajia matokeo makubwa.
Amesema kwa sasa ameamua kupita njia tofauti ikiwemo
kurudisha strategy za muziki wa zamani, ambapo msanii alikuwa akiweka nguvu
zote kwenye audio kwanza, bila kutarajia kuwa video itambeba.
kuwa, miaka ya hivi karibuni kufuatia
mapinduzi ya video za gharama, ambayo kimsingi yeye ndiye alikuwa muasisi,
wasanii wengi wamekuwa wakiumiza vichwa zaidi kufanya video kubwa na wengine
bila kuzingatia sana uzito wa audio yake. Hicho ni kitu anasema kwa sasa
hakizingatii tena.
“Siku hizi watu wanajaji ngoma kwa video kuliko audio.
Kwahiyo sasa hivi najaribu kurudi kule kwa 2008 kurudi nyuma, vile ambavyo
tulikuwa tunafanya zamani,”
“Nataka kuirudisha ile strategy ya zamani, ili watu
waconcentrate zaidi kwenye audio, yaani unaenda kwenye redio watu hawasifii
audio wanasifia video zaidi. Fanya audio iwe kali halafu unafanya video kali,”
amesisititiza.
Hivi karibuni AY aliachia single mpya iitwayo More &
More aliyomshirikisha Nyashinski.
No comments:
Post a Comment