BILIONI 93 KUINUSURU MIUNDOMBINU YA HALMASHAURI YA ILALA - boazmwakasege.com

MADA MOTO

Thursday, August 4, 2016

BILIONI 93 KUINUSURU MIUNDOMBINU YA HALMASHAURI YA ILALA


Suala la Miundombinu kwa jiji la Dar es Salaam ni kitendawili ambacho kinazua majibu mapya kila siku, baadhi ya barabara zimekuwa zikijengwa chini ya kiwango na wakandarasi na kuzirudia barabara hizo, kwa upande wa halmshauri ya Ilala kupitia baraza la madiwani wamepata mwarobaini wa suala hilo.


Akizungumza jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani Mstahiki Meya Charles Kuyeko ameeleza kuwa kufuatia malalamiko ya madiwani kuhusu suala la miundombinu kwa maeneo ya Halmashauri hiyo, Mstahiki Meya ameeleza kuwa wamehadiwa kupatiwa bilioni 93 na benki ya dunia endapo wataweza kulipa kiasi cha shilingi milioni 8 zitakazo tumika kuwalipa wananchi ambao wamejenga maeneo yaliyo katika hifadhi ya barabara.


Mstahiki Meya Kuyeko ameendelea kufafanua kuwa tayari wameisha kopa  kiasi hicho cha fedha hivyo wapo mbioni kuanza zoezi hilo la ukarabati wa mindombinu ya barabara kwa kiwango kinachostahili na mifereji ya maeneo mbalimbali, na Mkururugenzi wa Halmashauri hiyo Msongela Nitu ameahaidi kushirikiana na baraza la madiwani kwa masuala yote yenye tija kwa watanzania.


Huku kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Ukonga Bona Kaluwa akiiomba serikali kulitafutia ufumbuzi suala la kupunguziwa vyanzo vya mapato kwa Halmashauri hiyo jambo ambalo linawawia vigumu kama wajumbe wa baraza la madiwani kutekeleza baadhi ya miradi ya maendeleo ukizingatia kuwa shughuli nyingi za serikali zinafanyika Ilala kutokana na uwepo wa Ikulu.


No comments:

Post a Comment