AJIBU AWEKA REKODI SIMBA!! - boazmwakasege.com

MADA MOTO

Friday, August 5, 2016

AJIBU AWEKA REKODI SIMBA!!


MSHAMBULIAJI Ibrahim Ajibu, juzi alifikisha mabao matano ya kufunga ndani ya mechi tatu za kirafiki za kujipima nguvu za timu yake ambayo imeweka kambi Chuo cha Biblia mjini Morogoro kujiandaa na msimu mpya.
Mshindi huyo wa tuzo ya Bao Bora la Msimu uliopita wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, juzi aliifungia Simba mabao mawili wakati ikiilaza 5-0 dhidi ya Burkina Fasso ya Morogoro katika mchezo wa kirafiki uliopigwa Uwanja wa Highlands, Bigwa mkoani humo.
Mabao mengine ya Simba inayofundishwa na Kocha Mcameroon, Joseph Omog, yalifungwa na viungo Said Ndemla na wachezaji wapya, Mussa Ndusha kutoka DRC na Shiza Kichuya kutoka Mtibwa Sugar.

Ajibu ambaye mashabiki wake wanamuita ‘Cadabra’ wakimfananisha na mshambuliaji mpya wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic, awali alifunga bao moja katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Moro Kids na mawili katika ushindi wa 6-0 dhidi ya Polisi Morogoro.


Simba SC itashuka tena dimbani Agosti 8, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kumenyana na Interclube ya Angola katika mchezo wa kuazimisha miaka 80 ya klabu hiyo, maarufu kama Simba Day

No comments:

Post a Comment