Lulu aeleza mapinduzi yanayoletwa na filamu yake mpya ‘Ni Noma’ inayotoka Ijumaa hii - boazmwakasege.com

MADA MOTO

Wednesday, July 13, 2016

Lulu aeleza mapinduzi yanayoletwa na filamu yake mpya ‘Ni Noma’ inayotoka Ijumaa hii

Lulu Liz

Filamu hiyo inaingia sokoni Ijumaa hii kwa mfumo wa dijitali ambapo watu watainunua na kuingalia kwenye smartphone zao kupitia app ya Proin Box.

Lulu ameiambia MWAKASEGE BLOG kuwa filamu hiyo imekuja na mapinduzi makubwa kwa kila kitu kuanzia teknolojia na uigizaji. Amedai kuwa yeye na kampuni yake ya Proin, walitaka kuja na kitu tofauti na vilivyozoeleka kwenye filamu za Tanzania.


“Ilitubidi kwa kiasi fulani tutulie, tusome mazingira, tasnia yetu inamiss nini sasa hivi, mashabiki wetu wanahitaji nini sasa hivi,” anasema Lulu.
“Tumejitahidi kufanya production ya tofauti ambayo ina quality nzuri, it needs time, sio kama zamani kwa siku mnaweza mkashoot scene sita, saba, lakini saa zingine production kwa siku tulikuwa tunaweza kushoot scene mbili tu lakini mnahakikisha mnatoka na kitu kizuri,” ameongeza.

Amedai kuwa hata sauti zingine pia ilibidi waziingize upya studio ili kuwa na kitu bora kama ambavyo hufanyika kwenye filamu za Hollywood.




KAMA ULIPITWA NIMEKUSOGEZEA, WIMBO MPYA WA DIAMOND PLATNUMZ FT P SQUARE UMEVUNJA #RECORD BONYEZA HAPA CHINI KUONA!!

No comments:

Post a Comment