Matumla amestaafu ngumi? - boazmwakasege.com

MADA MOTO

Saturday, January 28, 2017

Matumla amestaafu ngumi?

Related image

Baada ya kupotea kwa muda mrefu katika ulingo wa masumbwi, bingwa wa zamani wa dunia wa I.B.O Mbwana Matumla amesema bado hajastaafu ngumi na kuwataka mashabiki wake waje kuona ufundi mpya aliokuja nao wakati atakapomvaa Shaban Selemani katika pambano la raundi sita litakalochezwa Februari tano katika uwanja wa ndani wa taifa jijini Dar es Salaam.

Mkali huyo anayetokea katika familia ya masumbwi na kuwahi kutamba ndani na nje ya nchi na kuwahi kutwaa mikanda ya ubingwa wa WBA,IBO,ICB na Asian Pacific amesema hajafikiria kustaafu kucheza ngumi kwa kuwa bado ana uwezo kuendelea kupambana ulingoni hivyo amewataka mashabiki wake kufika kwa wingi siku hiyo kujionea ufundi mpya alioibuka nao kutoka mafichoni.


Mbwana atacheza pambano hilo lisilo la ubingwa likiwa ni la utangulizi huku pambano kubwa litakuwa ni kati ya Ramadhani Shauri dhidi ya Meshack Mwankemwa la kuunganisha mikanda ya taifa wa TPBC na wa Afrika Mashariki na kati ambapo leo matumla amepata fursa ya kucheza Sparing dhidi ya bondia Mwankemwa.

No comments:

Post a Comment