NATAKA JIJI LA MBEYA LIWE LA MFANO KWA USAFI HAPA NCHINI-RC MBEYA - boazmwakasege.com

MADA MOTO

Monday, July 11, 2016

NATAKA JIJI LA MBEYA LIWE LA MFANO KWA USAFI HAPA NCHINI-RC MBEYA


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala ametangaza operesheni ya usafi na utekelezaji wa sheria ndogo za jiji zilipitishwa tangu mwaka 2014 ili kulifanya jiji hilo kuwa moja ya majiji safi hapa nchini

Hayo ameyasema leo baada ya kukagua magari 6 ya taka na makontena 91 ya kubebea taka na kuongea na madiwani, watendaji wa mara na mitaa na kuwataka kusimamia sheria na vifaa walivyopata kuhakikisha jiji hilo Lina kuwa safi wakati wote
"Magari tumepata, sheria ndogo ndogo zipo, adhabu kwa watupa taka zipo, adhabu kwa watiririshaji Maji machafu zipo, nyie viongozi na watendaji mpo sasa tukasimamie sitaki visingzio na nitapita kila maeneo mahali ambapo pana uchafu tutaanza na sisi tuliopo hapa nataka jiji safi na la mfano Tanzania"

No comments:

Post a Comment