Waziri Mkuu Apiga Marufuku wanafunzi kutumia viberit na mishumaa mabwenini - boazmwakasege.com

MADA MOTO

Sunday, July 17, 2016

Waziri Mkuu Apiga Marufuku wanafunzi kutumia viberit na mishumaa mabwenini

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku matumizi ya viberiti, mishumaa na hita za kuchemshia maji kwa wanafunzi wa bweni ili kuepusha majanga ya moto na atakayekutwa, atachukuliwa hatua kali.

“Kuna tabia ya baadhi ya wanafunzi hasa wa masomo ya fizikia kutengeneza vifaa vya kienyeji vya kuchemsha maji mabwenini, jambo hili ni la hatari kwani linaweza kusababisha ajali ya moto, hivyo ni marukufu kwa mwanafunzi kutumia vifaa hivyo,” alisema.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana katika harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa majengo ya Shule ya Sekondari Lindi, yaliyoungua moto usiku wa kuamkia Julai 10, mwaka huu.


Katika ajali hiyo shule imeathirika kwa asilimia 34 baada ya vyumba tisa vya madarasa, jengo lenye matundu 26 ya vyoo na jengo la maabara ya kemia na fizikia yameungua na kusababishia hasara ya Sh milioni 682.78.


KAMA BADO HAUJAONA HII HAPA HUKO INDIA WANAUME WATAMBIANA KWA KUKATA MAUNO, 

VIDEO :

No comments:

Post a Comment