Marekani Yakana Kuhusika na Mapinduzi Uturuki - boazmwakasege.com

MADA MOTO

Sunday, July 17, 2016

Marekani Yakana Kuhusika na Mapinduzi Uturuki

Marekani imeitaka Uturuki kujizuia baada ya jaribio la mapinduzi lililozimwa siku ya Ijumaa ambapo maelfu ya maafisa wa kijeshi wamekamatwa.

Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni nchini Marekani John Kerry ameutaka utawala nchini Uturuki kuheshimu sheria wakati wa uchunguzi wao kuhusu mapinduzi hayo.

Kerry amesema kuwa madai kwamba Marekani ilihusika katika mapinduzi hayo inasababisha madhara kwa uhusiano kati ya washirika hao wawili wa NATO.


 Mapema kupitia kwa hotuba yake, rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan alitoa wito kwa rais Obama kumrejesha nchini humo kiongozi wa kidini raia wa Uturukli anayeishi nchini humo Fethullah Gulen ambaye analaumiwa kwa kupanga mapinduzi hayo.

JE ULIMISS VIDEO TAMU YA WHATSAP VITUKO?? HII HAPA MTU WANGU BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA!

No comments:

Post a Comment