Mgogoro unaoiandama CUF huenda ukailetea balaa zaidi, baada ya kuwapo kwa taarifa kuwa huenda ikafutwa kama itazidi kukomalia msimamo ilionao wa kutotaka ushauri.
Mgogoro huo umekipasua chama hicho na kuwa makundi mawili, moja likiongozwa na Profesa Ibrahim Lipumba na jingine likiwa chini ya Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad.
Profesa Lipumba aliyevuliwa uanachama na Baraza Kuu la Uongozi amejitwalia ofisi kuu za chama hicho zilizopo Buguruni jijini Dar es Salaam, wakati Maalim Seif na wanaomuunga mkono wako makao makuu ya chama hicho Vuga visiwani Zanzibar.
CHANZO: MTEMBEZI.COM
No comments:
Post a Comment